Kassim Mganga akimbia na hela za studio

Soudy Brown wa Clouds fm ana story hii ya kutokea ugomvi kwenye studio moja Dar kulitokea mtafaruku uliowahusisha wasanii wawili huku chanzo kikidaiwa kuwa ni fedha.

Mshiriki wa BBA 2012, ambae ni msanii  wa Bongo Fleva Julio amesema kulikuwa na kuto kuelewana kati ya management yake na ya Kassim Mganga, ambapo walikubaliano kufanya kazi na Kassim lakini wakati wa kukabidhiana kazi  hiyo aligundua studio hiyo imefanya kinyume na makubaliano yao kwa madai kuwa hela aliyotoa hawakuipata.

Julio amesema hela ya kulipia studio kwa ajili ya kufanya wimbo huo alimpatia Kassim, lakini studio wanasema hela haikufika.

Soudy Brown alimtafuta Kassim lakini hakujibu kitu chochote kuhusu hilo simu ikakatika.

Comments

Popular posts from this blog

hii ni list ya baadhi ya majina ya wasanii wa Nigeria waliohit mwaka huu kuanzia A-Z

mbinu za kuwa producer au mtayarishaji wa music