Posts

Showing posts from August, 2014

Jack Patrick apewa hukumu ndogo China

Image
BAADA ya kushikiliwa kwa takriban miezi tisa kwa kesi ya madawa ya kulevya ‘unga’, hatimaye Video Queen maarufu Bongo, Jacqueline Fitzpatrick Cliff ‘Jack Patrick’ amehukumiwa kifungo cha miaka 6 jela huku kukiwa na uwezekano wa kupunguziwa adhabu ikawa ndogo zaidi, Amani linaibumburua habari kamili. HUKUMU NYEPESI? Kwa mujibu wa mtu wa karibu wa Jack, modo huyo alihukumiwa Jumatatu iliyopita (Agosti 11, mwaka huu) kwenye Mahakama ya Macau huko Hong Kong ambapo hukumu hiyo ilitofautiana na adhabu nyingine za madawa nchini humo ambazo huwa hukumu yake ni kunyongwa hivyo ya Jack kuonekana nyepesiii! KWA NINI NYEPESI? Kikimwaga data, chanzo hicho makini kilidai kwamba, hukumu hiyo ya Jack ni nyepesi ukilinganisha na hukumu nyingine za madawa ya kulevya zinazotolewa nchini China ambapo hakimu alitumia muda wa dakika 27 tu kuisoma. “Hukumu za madawa ya kulevya zinatofautiana nchini China. Kuna baadhi ya majimbo kama Beijing huwa wao ikithibitika umebeba madawa ya kulevya, una

Wood ajiondoa katika kombe la Ryder

Image
Tiger Wood ajiondoa mashindano ya kombe la Ryder Mchezaji nyota wa gofu Tiger Wood wa Marekani, amejiondoa katika mashindano ya kombe la Ryder baada ya kushauriwa na madaktari wake. Tiger amekuwa akisumbuliwa na maumivu ya mgongo mara kadhaa na kufikia usiku wa kuamkia hii leo ameamua kutangaza kujitoa kwenye michuano hiyo ya kimataifa. Tiger amemuomba kocha wa timu ya Taifa ya Marekani Tom Watson amuwie radhi kwani wataalamu wake wa Afya wamemtaka apumzishe mgongo wake wenye matatizo na hata wamemzuia asifanye mazoezi yeyote.

fasheni zilizopo sokoni

kliniki ya kusaidia watu kujiua

Takribani waingereza 800 ambao wamechoka maisha waliyo nayo kutokana na kusumbuliwa na magonjwa mbali mbali wamejiunga kwenye foleni ya kusubiria kifo katika kliniki ya Diginitas ya nchini Uswizi. Taarifa za magazeti ya Uingereza zilisema kwamba waingereza 800 ambao wanasumbuliwa na magonjwa mbali mbali ambayo hayana tiba ambao wanataka wafariki muda wowote baada ya kuchoka maisha waliyonayo wamejiorodhesha kwenye foleni ya kusaidiwa kujiua kwenye kliniki ya Diginitas iliyopo nchini Uswizi. Uswizi ndio nchi pekee ya ulaya ambayo inaruhusu watu kusaidiwa kujiua pale wanapoona magonjwa yao ambayo hayana tiba yanawatesa kwa muda mrefu. Kliniki ya Diginitas huwasaidia watu wanaotaka kujiua kwa kuwapa dozi kubwa za madawa ambazo husimamisha mapigo yao ya moyo na kuwaua taratibu wakiwa wamelala. Watu wengi ambao hujiua kwenye kliniki hiyo ni wale ambao wanasumbuliwa na magonjwa yasiyotibika kama vile kansa na mengineyo ambayo huwa yamefikia hatua za mwisho mwisho. Ni kosa la jinai kumsaidia

treni la Uswiswi lapata ajali

Image
Treni lililobeba abiria zaidi ya 200 limepata ajali kwa kutereza pembeni ya reli na kusababisha baadhi ya mabehewa kuwa nje ya reli. Abiria waliokuwemo ndani ya treni hilo walilazimika kukimbilia upande wa pili wa treni hilo ili kuepuka lisidondoke kwenye maporomoko.  Juhudi hizo zilisaidia na hakuna mtu aliyefariki kwenye hiyo ajali lakini watu 11 walipata majeraha na watano kati yao kupata majeraha makubwa. Ajali hii imetokea kwenye mlima ya nchini Uswisi toa maoni yako

mashindano ya karate ya dunia kufanyika Tanzania

Image
Katibu Mkuu wa UPAM Tanzania Joe Jolamu (kushoto) akingea na waandishi wahabari leo jijini Dar es salaam juu ya mashindano ya karate ya dunia yanayotarajiwa kufanyika nchini mwishoni mwa mwaka huu au mwanzoni mwakani. Kulia ni Rais wa UPAM duniani Prof. Maurizi Mardina. R ais wa UPAM duniani Prof. Maurizi Mardina akimshikilia shingo Master Hudu Thabit akionesha moja ya mbinu inazotumika kwa kujihami kwa ajili ya usalama. Rais wa UPAM duniani Prof. Maurizi Mardina (kushoto) baada ya kuonesha mbinu ya kujihami kwa mwandishi wa habari Kibwana Dachi (aliyekaa). Kulia ni Master Hudu Thabit. Umoja wa Wapiganaji wa Sanaa ya Mapigano Duniani (UPAM) unaandaa shindano la kimataifa la wapiganaji ambalo linatarajiwa kufanyika nchini kati ya Mwezi Desemba mwaka huu na mwanzoni mwa mwaka ujao kutokana na ruhusa itakayotolewa na Serikali kwa mamlaka zinazohusika. Kauli hiyo imetolewa leo na Rais wa UPAM Prof. Maurizi Mardina alipokuwa akiongea na waandishi wa habari jijini Dar

TFF haitambui mabadiliko ya uongozi Coastal Union

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) halitambui mabadiliko ya uongozi ndani ya Coastal Union yanayodaiwa kufanywa na mkutano wa wanachama wa klabu hiyo uliofanyika hivi karibuni. Uongozi wa Coastal Union uliochaguliwa na mkutano wa uchaguzi wa klabu hiyo ndiyo ambao tunautambua, na tutaendelea kufanya nao kazi, na sio uongozi mwingine wowote ule. Tunapenda kuwakumbusha wanachama wetu (ikiwemo Coastal Union) kuheshimu katiba ya TFF pamoja na katiba zao, kwani hazitambui mapinduzi ya uongozi wala kamati za muda za utendaji. TFF inafanya kazi za kamati za utendaji zilizopatikana kwa njia ya uchaguzi tu. Tayari tumepokea barua kutoka kwa Kaimu Mwenyekiti wa Coastal Union, Steven Mnguto ikilalamikia kusimamishwa kwake. Hivyo, tunafuatilia suala hilo kwa kina, na ikibainika kuwa kuna viongozi wamehusika katika mapinduzi hayo watafikishwa katika vyombo husika kwa hatua zaidi.

mwanariadha Montsho yupo mbioni kupigwa marufuku

Image
Mwanariadha bingwa wa zamani wa dunia wa mita 400 Amantle Montsho anakabiliwa na marufuku ya miaka miwili kutoshiriki michezo hiyo, baada ya kugundulika kutumia dawa za kuongeza nguvu wakati wa michezo ya Jumuia ya madola. Mwanariadha huyo wa Botswana mwenye umri wa miaka 31, ambaye alimaliza mashindano hayo kwa kuwa mshindi wa nne, anatakiwa mpaka Agosti 22 awe amekata rufaa katika Shirikisho la michezo ya Jumuia ya Madola CFG. Shirikisho hilo limeyapeleka matokeo ya vipimo hiyo kwa mashirikisho mengine ya michezo ya kimataifa, ambayo pia yanaweza kumpiga marufuku mwanariadha huyo kushiriki. Mike Hooper, Mkurugenzi mtendaji wa CFG, amesema mwanariadha huyo amejulishwa kuhusiana na matokeo ya vipimo hivyo na kwamba anahaki ya kuweza kujibu mpaka ifikapo Ijumaa Agosti 22. Shirikisho hilo linauwezo tu wa kubatilisha matokeo ya Montsho katika michezo hiyo, kufuatia kugundulika kutumia dawa. Iwapo atatiwa hat

top 10 ya wasanii matajiri Africa

10. Jose Chameleone Jose (or Joe) Chameleone is a Ugandan artiste who found his niche blending traditional Ugandan folk music, a bit of rumba and a heavy reggae influence. He sings in English, Swahili and Luganda. His mansion outside of Kampala and four cars (including a Cadillac Escalade and a Benz) are evidence of his success, particularly with his hit, ValuValu. He's been credited with changing the face of music in Uganda, as well as making local music accessible to the rest of the world. 9. Banky W Born Olubankole Wellington in the U.S, Banky W moved back to Nigeria and grew up in Lagos, where he began singing at an early age. Finding success early in singing competitions, most of his wealth has come from endorsement deals with companies such as Etisalat mobile and Samsung in Nigeria. He also started the Mr Capable Foundation, an education charity that provides tuition scholarships for disadvantaged children. 8. Hugh Masekela Musical sensation Hug

pesa nyingine hizoo daraja la kivukoni

Image
Waziri wa Ujenzi John Magufuli amesema Serikali inatarajia kuongeza kivuko kingine cha kuvusha watu Kigamboni ambacho kitagharimu shilingi bilioni 3.7 wakati ujenzi wa daraja ukiendelea. Anasema daraja linalojengwa sasa hivi litakamilika June 2015 badala ya July kama ilivyokua imefahamika mwanzoni ambapo tayari Mkandarasi ameshalipwa shilingi Bilioni 117 kati ya 214 za kukamilisha mradi wote limeandika gazeti la Tanzania Daima. Nalo gazeti la HabariLEO August 9 2014 limeandika >> Magufuli abana wenye magari Kigamboni, ataka wasisumbue abiria wa Pantoni asubuhi na jioni, wenye haraka watakiwa kuzunguka Kongowe – Mbagala, ni agizo la muda mfupi baada ya kivuko kilichopo kuzidiwa. chanzo millardayo.com

machache kuhusu Christian Bella

Image
  Jina lake halisi ni Christian Bella raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC). Bendi yake pia imekuwa maarufu lakini yeye ndiye anayevuma zaidi kutokana na kwamba kazi nyingi zinazofanya vizuri ni zake na hata asipokuwepo pengo linaonekana, wanaokwenda kwenye maonyesho ya bendi hiyo jijini Dar es Salaam hata mikoani watakuwa mashuhuda wa hilo. Ndiyo bendi ambayo kwa sasa inajaza zaidi kwenye maonyesho yake ukilinganisha na bendi nyingine ambazo ni maarufu na kongwe kuliko Malaika. Baadhi ya nyimbo za Bella zinazotamba kwa sasa ni ‘Nakuhitaji’, ‘Usilie’, ‘Msaliti’,‘Nani kama Mama’. Kikubwa kingine kilichombeba msanii huyo na bendi yake kwa sasa kuwa na nyimbo nyingi nzuri na zinazofahamika na mashabiki tofauti na bendi zingine. Lakini hata hivyo, rekodi inambeba msanii huyo kwa vile alipotua Akudo Impact alifanya vizuri na kung’ara na nyimbo alizotunga kama ‘Yako wapi Mapenzi’, ‘Bomoabomoa’ na ‘Safari Siyo Kifo’. “Kila mahali kuna changamoto zake, Akudo k

Kinondoni kukamilisha ratiba ya Ligi ya Kikapu

KANDA ya Kinondoni ndio ya mwisho katika kukamilisha ratiba ya kupata timu nne zitakazoshiriki Ligi ya Mpira wa Kikapu Mkoa wa Dar es Salaam (RBA) inayotarajia kuanza mapema mwezi ujao. Rais wa Chama cha Mpira wa Kikapu Mkoa wa Dar es Salaam (BD), Richard Jules, alisema kuwa Kinondoni itaanza ligi yao leo Jumamosi ambayo itashirikisha timu nane. Alizitaja timu hizo kuwa ni Oilers, Pazi, Magnets, UDSM Outsiders, Crows, Mabibo Bullets, Don Bosco na Chui, wakati Kanda ya Temeke na Ilala tayari zilipata wawakilishi wake. “RBA msimu ujao itakuwa na timu 12 ambapo kila kanda itatoa timu nne, Temeke na Ilala walifanya ligi yao lakini Kinondoni hawakufanya kwa sababu ya kupisha mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan. “Baadhi ya timu kutoka Temeke ni ABC na JKT Stars na Ilala ni Vijana na Savio wakati upande wa wanawake wao hawashiriki ligi ndogo kwa sababu timu zipo chache hivyo wanaingia moja kwa moja kwenye ligi,” alisema Jules.

picha za jana kwenye tamasha la matumaini 2014

Image
wasanii wa Maigizo,Cloud (kushoto) na JB, wakichana wakati wa Tamasha hilo. Jb alishinda kwa Pointi.  KWA MATUKIO KAMILI YA PICHA ZA TAMASHA HILI KAA NASI HAPO BAADAYE.     Msanii wa kunyanyua vitu vizito, Maisala Juma akionyesha umahiri wake wa kufanya mazoezi wakati wa Tamasha la Matumaini lililodhaminiwa na Vodacom Tanzania katika kuazimisha sikukuu ya Nanenane katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam jana. Msanii wa muziki wa    nyimbo za dini    kutoka mbeya Bw. Ambwene Mwasongwe,akiimba na kukongonga nyoyo za mashabiki wa nyimbo zake wakati wa Tamasha la Matumaini lililodhaminiwa na Vodacom Tanzania katika kuazimisha sikukuu ya    Nanenane katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam jana. Kikosi cha Bongo Movie kilichokikabili kikosi cha Bongo wakati wa Tamasha la Matumaini lililoandaliwa na Global Publishers na kudhaminiwa na Vodacom Tanzania katika kuazimisha sikukuu ya    Nanenane katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam jana. Msanii wa Muzi

Kibonde wa crouds fm ndani ya kibindo kikali na traffic

Image
Mtangazani Mahiri wa Redio Clouds FM Ephrahim Kibonde akidhibitiwa na Askari wa Usalama barabarani. Mtangazani Mahiri wa Redio 88.5 Clouds FM kupitia kipindi cha Jahazi, Ephrahim Kibonde akidhibitiwa na Askari wa Usalama barabarani wakati alipotakiwa kutii sheria bila shurti,mapema asubuhi hii jijini Dar es salaam. Kibonde anadaiwa kusababisha ajali asubuhi hii eneo la Makumbusho, ikiwa gari aliyokuwa akiendesha kuigonga gari ya dereva mwingine kwa nyuma. Trafiki walifika eneo la tukio na kupima ajali, Kibonde alipoona hivyo akarudi nyuma na kuendesha gari lake kuondoka eneo la tukio bila kufuata taratibu za usalama barabarani,hali iliyomlazimu yule Trafiki katumia gari lililogongwa kumfukuzia.… Mtangazani Mahiri wa Redio Clouds FM Ephrahim Kibonde akidhibitiwa na Askari wa Usalama barabarani. Mtangazani Mahiri wa Redio 88.5 Clouds FM kupitia kipindi cha Jahazi, Ephrahim Kibo

Tulirubuniwa tuwaue Dk. Slaa, Mnyika

Image
Madiwani walioasi Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) wamerejea na kudai walirubuniwa na makada watano wa CCM kuhama kwenye chama hicho ili wawatumie kuwaua, Dk. Willbrod Slaa na John Mnyika.   Madiwani hao ni Sebastian Mzuka wa kata ya Ngokolo na Zacharia Martin wa kata ya Masekelo wote kutoka Shinganya mjini ambao wamewataja makada hao kuwa ni Naibu wa Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana.   Wengine ni Naibu waziri wa Nishati na Madini, Steven Masele ambaye pia ni Mbunge wa Shinyanga mjini, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa NEC, chama tawala, Nape Nnauye, na Habibu Mchange (aliyefukuzwa Chadema).   Wakizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam katika ofisi za chama hicho, madiwani hao walisema kuwa, mauaji hayo yalipangwa kutekelezwa kwa kiasi cha Sh. milioni 180.   Diwani Mzuka alisema wamefika kwenye ofisi hizo ili kueleza kinachoendelea kudhoofisha chama na kuomba toba baada ya  kuhama.   Ali

RAIS KIKWETE ATEMBELEA MAKTABA YAKIRAIS YA GEORGE W. BUSH JIJINI DALLAS, TEXAS

Image
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete wakitembelea Maktaba ya Kirais ya Rais Bush (Bush Presidential Library) iliyo katika Taasisi ya Bush (George W. Bush Institute) mjini Dallas, Texas, na kujionea nafasi kubwa iliyotolewa kwa Tanzania na zawadi ambazo Rais Bush alizipata katika ziara yake rasmi ya Tanzania wakati akiwa Rais wa Marekani.  Maktaba hiyo ya kuvutia inaendeshwa kwa teknolojia ya kisasa kabisa ya habari na mawasiliano. Rais Kikwete alikuwa amesimama mjini Dallas kwa muda akiwa njiani kutoka Washington D.C., kwenda Houston, jimbo hilo hilo la Texas kuhudhuria mkutano wa wafanyabiashara wa mafuta na gesi ambao wanataka kuwekeza katika sekta hiyo katika Tanzania.   Rais Kikwete amekuwa katika Marekani kwa ziara ya kikazi ya siku tisa, ambako miongoni mwa mambo mengine, amehudhuria Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Marekani na Afrika uliofikia kilele chake jana kwa kikao kilichoendeshwa na Rais Barack Obama wa Marekani katika Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani

Ghana ipo kwenye hatari ya kupigwa marufuku ya FIFA

Image
Ghana inakabiliwa na tishio la kupigwa marufuku na shirikisho la soka duniani FIFA baada ya serikali kuanzisha uchunguzi wa matokeo duni katika kombe la dunia huko Brazil. The Black stars ya Ghana ilimaliza na alama moja pekee katika kundi G baada ya kucheza mechi tatu . Aidha kampeini yao huko Brazil ilikumbwa na misukosuko ya nidhamu na migomo ya malimbikizi ya marupurupu ya wachezaji. FIFA imeipatia onyo shirikisho la soka la Ghana kuikumbusha kuwa inakiuka kanuni za shirikisho hilo kwa kuruhusu au kushiriki uchunguzi wa aina yeyote kuhusiana na matokeo duni katika mchuano wa kombe la dunia huko Brazil. Muntari na Boateng wakijivinjari baada ya kutimuliwa kambini Kwa wakati mmoja rais wa Ghana John Mahama alilazimika kuingilia kati na kutuma zaidi ya dola milioni tatu za Marekani ilikuzuia mgomo wa wachezaji kufuatia malimbikizi ya marupurupu. Rais Mahama baadaye aliagiza

Arsenal kimbembe na Besikitas

Kilabu ya Uingereza Arsenal itachuana na kilabu ya Besikitas ya Uturuki katika mechi za mchujo wa kombe la Mabingwa,huku Celtic ya Scotland ikikabana koo na mabingwa wa Slovenia Maribor baada ya kilabu hiyo kurudishwa katika mechi hizo. Arsenaly imekuwa ikishiriki katika mechi za mchujo wa kombe hilo katika kipindi cha miaka 16 iliopita. Kilabu ya Celtic ilipoteza kwa mabao 6 kwa moja dhidi ya Legia Warsaw katika michuano ya kufuzu kwa dimba hilo,lakini mabingwa hao wa Poland wakaondolewa kwa kushirikisha mchezaji ambaye hakufaa kucheza. Katika Ligi ya bara Yuropa Totenham ya Uingereza itapimana nguvu na AEL Limassol ya Cyprus huku Hull City ikichuana na kilabu ya Lokeren kutoka Ubelgiji. Kilabu ya Besikitas ilimaliza ya tatu katika jedwali la ligi ya Uturuki na wanafunzwa na aliyekuwa kocha wa kilabu ya West Ham pamoja na mlinzi wa zamani wa Everton Slaven Bilic na kikosi chao kinashirikisha aliyekuwa ms