machache kuhusu Christian Bella

 
Jina lake halisi ni Christian Bella raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC). Bendi yake pia imekuwa maarufu lakini yeye ndiye anayevuma zaidi kutokana na kwamba kazi nyingi zinazofanya vizuri ni zake na hata asipokuwepo pengo linaonekana, wanaokwenda kwenye maonyesho ya bendi hiyo jijini Dar es Salaam hata mikoani watakuwa mashuhuda wa hilo.
Ndiyo bendi ambayo kwa sasa inajaza zaidi kwenye maonyesho yake ukilinganisha na bendi nyingine ambazo ni maarufu na kongwe kuliko Malaika.
Baadhi ya nyimbo za Bella zinazotamba kwa sasa ni ‘Nakuhitaji’, ‘Usilie’, ‘Msaliti’,‘Nani kama Mama’. Kikubwa kingine kilichombeba msanii huyo na bendi yake kwa sasa kuwa na nyimbo nyingi nzuri na zinazofahamika na mashabiki tofauti na bendi zingine.
Lakini hata hivyo, rekodi inambeba msanii huyo kwa vile alipotua Akudo Impact alifanya vizuri na kung’ara na nyimbo alizotunga kama ‘Yako wapi Mapenzi’, ‘Bomoabomoa’ na ‘Safari Siyo Kifo’.
“Kila mahali kuna changamoto zake, Akudo kulikuwa na changamoto ambazo naweza kukumbana nazo sehemu nyingine, hivyo ni jambo la kawaida, naweza kusema kwamba niliondoka Akudo bila kugombana na mtu, nilitaka kuendesha mambo yangu mwenyewe,” anaeleza Bella katika mahojiano maalumu kwenye ofisi za Mwanaspoti, Tabata Relini jijini Dar es Salaam.
“Mwaka 2012 nilienda Sweden kwa mke wangu ambaye alikuwa anajifungua hivyo nililazimika kuwepo ili kushuhudia mtoto wangu akizaliwa, nilishuhudia kila kitu na sasa nina watoto wawili wa kiume Jordan (7) na Hance (2).
“Nikiwa huko nilitunga wimbo ulioitwa ‘Msaliti’ ambao niliutuma hapa nchini na ulifanya vizuri, niliporudi nikawa mwanamuziki wa kujitegemea na kupata shoo zote za Fiesta ambapo mwanamuziki wa dansi nilikuwa peke yangu,” anaongeza.
Chanzo cha wimbo wa Nani Kama Mama
“Niliamua kutunga wimbo huu baada ya kushuhudia hatua zote mke wangu alipojifungua, kiukweli mwanamke anatakiwa kuheshimika tofauti na wanavyowachukulia, hapo ndipo niliona kuna haja ya kuimba wimbo wenye ujumbe huu.
“Hata katika uzinduzi wangu nimeupa jina la Usiku wa Mama ni maalumu kwa akina mama wote duniani, uzinduzi ambao nitaufanya Mzalendo Pub, Agosti 29, mwaka huu,” anasema Bella ambaye katika wimbo huo amemshirikisha Mwanamuziki wa Bongo Fleva, Ommy Dimpoz.

Comments

Popular posts from this blog

hii ni list ya baadhi ya majina ya wasanii wa Nigeria waliohit mwaka huu kuanzia A-Z

mbinu za kuwa producer au mtayarishaji wa music