mwanariadha Montsho yupo mbioni kupigwa marufuku
Shirikisho hilo limeyapeleka matokeo ya vipimo hiyo kwa mashirikisho mengine ya michezo ya kimataifa, ambayo pia yanaweza kumpiga marufuku mwanariadha huyo kushiriki.
Mike Hooper, Mkurugenzi mtendaji wa CFG, amesema mwanariadha huyo amejulishwa kuhusiana na matokeo ya vipimo hivyo na kwamba anahaki ya kuweza kujibu mpaka ifikapo Ijumaa Agosti 22.
Shirikisho hilo linauwezo tu wa kubatilisha matokeo ya Montsho katika michezo hiyo, kufuatia kugundulika kutumia dawa.
Iwapo atatiwa hatiani, Montsho atapelekwa katika Shirika la Kimataifa la kupambana na madawa ya kuongeza nguvu michezoni WADA, pamoja na mashirika maengine kwa ajili ya kukabiliwa na vikwazo zaidi.
Comments
Post a Comment