kliniki ya kusaidia watu kujiua

Takribani waingereza 800 ambao wamechoka maisha waliyo nayo kutokana na kusumbuliwa na magonjwa mbali mbali wamejiunga kwenye foleni ya kusubiria kifo katika kliniki ya Diginitas ya nchini Uswizi. Taarifa za magazeti ya Uingereza zilisema kwamba waingereza 800 ambao wanasumbuliwa na magonjwa mbali mbali ambayo hayana tiba ambao wanataka wafariki muda wowote baada ya kuchoka maisha waliyonayo wamejiorodhesha kwenye foleni ya kusaidiwa kujiua kwenye kliniki ya Diginitas iliyopo nchini Uswizi.

Uswizi ndio nchi pekee ya ulaya ambayo inaruhusu watu kusaidiwa kujiua pale wanapoona magonjwa yao ambayo hayana tiba yanawatesa kwa muda mrefu.

Kliniki ya Diginitas huwasaidia watu wanaotaka kujiua kwa kuwapa dozi kubwa za madawa ambazo husimamisha mapigo yao ya moyo na kuwaua taratibu wakiwa wamelala.

Watu wengi ambao hujiua kwenye kliniki hiyo ni wale ambao wanasumbuliwa na magonjwa yasiyotibika kama vile kansa na mengineyo ambayo huwa yamefikia hatua za mwisho mwisho.

Ni kosa la jinai kumsaidia mtu kujiua nchini Uingereza.

Mtu anayemsaidia mgonjwa ambaye hajiwezi na hawezi kwenda mwenyewe kutoka Uingereza hadi Uswizi bila ya msaada wa mtu mwingine huingia kwenye fungu la watu wanaosaidia watu kujiua na hukabiliwa na kifungo cha miaka mingi jela.

Waingereza 34 ambao foleni yao imefika wako tayari kuelekea nchini Uswizi kwenye kliniki hiyo kuhitimisha maisha yao.

Idadi ya waingereza ambao wamejioredhesha kwenye foleni ya kusaidiwa kujiua kwenye kliniki hiyo kuanzia mwaka 2002 hadi sasa imeongezeka mara kumi zaidi.

Katika miezi 12 iliyopita Waingereza 23 walihitimisha maisha yao katika kliniki hiyo.
ni stori ya 2009

Comments

Popular posts from this blog

hii ni list ya baadhi ya majina ya wasanii wa Nigeria waliohit mwaka huu kuanzia A-Z

mbinu za kuwa producer au mtayarishaji wa music