Kinondoni kukamilisha ratiba ya Ligi ya Kikapu

KANDA ya Kinondoni ndio ya mwisho katika kukamilisha ratiba ya kupata timu nne zitakazoshiriki Ligi ya Mpira wa Kikapu Mkoa wa Dar es Salaam (RBA) inayotarajia kuanza mapema mwezi ujao.
Rais wa Chama cha Mpira wa Kikapu Mkoa wa Dar es Salaam (BD), Richard Jules, alisema kuwa Kinondoni itaanza ligi yao leo Jumamosi ambayo itashirikisha timu nane.
Alizitaja timu hizo kuwa ni Oilers, Pazi, Magnets, UDSM Outsiders, Crows, Mabibo Bullets, Don Bosco na Chui, wakati Kanda ya Temeke na Ilala tayari zilipata wawakilishi wake.
“RBA msimu ujao itakuwa na timu 12 ambapo kila kanda itatoa timu nne, Temeke na Ilala walifanya ligi yao lakini Kinondoni hawakufanya kwa sababu ya kupisha mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan.
“Baadhi ya timu kutoka Temeke ni ABC na JKT Stars na Ilala ni Vijana na Savio wakati upande wa wanawake wao hawashiriki ligi ndogo kwa sababu timu zipo chache hivyo wanaingia moja kwa moja kwenye ligi,” alisema Jules.

Comments

Popular posts from this blog

hii ni list ya baadhi ya majina ya wasanii wa Nigeria waliohit mwaka huu kuanzia A-Z

mbinu za kuwa producer au mtayarishaji wa music