Posts

Showing posts from November, 2014

ziwa nyasa bado ni utata kati ya Malawi na Tanzania

Baada ya kutokea vuta nikuvute kati ya nchi hizo mbili zilizokuwa marafiki wa miaka mingi, marais wastaafu kutoka Msumbiji, Joaquim Chissano, Festus Mogae wa Bostwana na Thabo Mbeki wa Afrika Kusini walipewa jukumu la kutafuta maridhiano. Kile kilichoonekana kuanza kama mzaha kati ya Tanzania na Malawi kuhusu umiliki wa Ziwa Nyasa, sasa kimeanza kuchukua sura mpya kwa kila nchi kuendelea kutekeleza kitu inachokiamini kuwa ni sahihi. Baada ya kutokea vuta nikuvute kati ya nchi hizo mbili zilizokuwa marafiki wa miaka mingi, marais wastaafu kutoka Msumbiji, Joaquim Chissano, Festus Mogae wa Bostwana na Thabo Mbeki wa Afrika Kusini walipewa jukumu la kutafuta maridhiano. Hivi karibuni marais hao walikutana na Rais Peter Mutharika kwa ajili ya kuzungumzia jambo hilo, lakini kwa bahati mbaya walichodhani kuwa ni jambo dogo, kiligeuka kuwa ‘mfupa mgumu’ baada ya rais huyo kusema Tanzania haimiliki hata inchi moja ya Ziwa Nyasa. Kama hiyo hai

Bibi harusi wa miaka 14 amuua mumewe kwa kupinga kuolewa

Bi harusi wa miaka 14 nchini Nigeria ameshtakiwa kwa kuwaua watu wanne akiwemo mumewe wa miaka 35 baada ya kuweka sumu ya panya katika chakula alichoandaa kwa sherehe za harusi yake. Kesi hiyo imewashangaza wanaharakati wa haki za kibinaadamu ambao wamesema kuwa msichana aliyeozwa kwa mume anayemzidi umri zaidi ya mara mbili yake anafaa kuchukuliwa kama mwathiriwa na wala siyo muhalifu Msichana huyo aliyetambulika kwa jina la Wasila Tasiu kutoka familia maskini katika eneo lenye idadi kubwa ya Waislamu huenda akakabaliwa na adhabu ya kifo Shahidi wa kwanza wa kiongozi wa mashtaka Lamido Abba Sorron-Dinka alikuwa msichana wa miaka 7 anayejulikana kama Hamziyya ambaye alikuwa akiishi katika nyumba moja na Tasi’u pamoja na mumewe Umar Sani wakati bi harusi huyo alipoweka sumu ya panya katika chakula hicho. Akizungumzia zaidi kuhusu kisa hicho ambacho kimevuta hisia za wengi msichana huyo wa miaka 7 alisema kwamba Tasi’u alimpa fedha ili kununua sumu ya panya kutoka d

sakata la Escrow Wabunge waungana

BUNGE la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jana lilikuwa moja dhidi ya utoaji wa fedha katika akaunti ya Tegeta Escrow katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT), huku baadhi ya mawaziri wakitofautiana na taarifa ya Serikali ya utetezi wa suala hilo. Kabla ya kuungana huko kwa wabunge, Mwenyekiti wa Kamati ya Fedha za Serikali (PAC), Kabwe Zitto alihitimisha hoja ya kamati hiyo na Bunge kuingia katika hatua ya kufanya uamuzi wa maazimio ya Bunge dhidi ya watuhumiwa wa uchukuaji wa fedha hizo. Awali kabla ya kufikia hatua ya maazimio, ambayo iliendelea mpaka jana usiku, Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba alikiri kuwa katika fedha zilizochotwa katika akaunti ya Tegeta Escrow katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT), kuna kodi ya Serikali na aliagiza wote walionufaika na fedha hizo kulipia kodi ifikapo Desemba 31, mwaka huu. Alisema Serikali ilipaswa kulipwa Sh bilioni 26.97, lakini hadi sasa imelipwa Sh bilioni 4.21. Akichangia mjadala kuhusu taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bun

Waliokufa na Ebola watimia 7,000

Takwimu mpya zilizotolewa na Shirika la Afya Duniani, WHO, zinaonesha kuwa watu karibu 7,000 wamefariki hadi sasa kutokana na Ebola, karibu wote Afrika Magharibi. Hao ni watu zaidi ya elfu moja kuliko idadi iliyotangazwa na WHO Jumatano tu. Vifo vingi zaidi vimesajiliwa Liberia. WHO inasema watu zaidi ya 16,000 wameugua Ebola hadi sasa. Waandishi wa habari wanasema kuongezeka kwa idadi ya waliokufa siyo lazima inamaanisha ugonjwa unazidi kutapakaa kwa kasi kwa sababu takwimu nyengine ni za zamani. Na Rais Francois Hollande wa Ufaransa amezuru Guinea, kiongozi wa kwanza asiyekuwa Muafrika kuzuru moja kati ya nchi tatu za Afrika Magharibi zilizoathirika sana na Ebola. Bwana Hollande alisema alitaka kuleta ujumbe wa matumaini kwa watu wa Guinea: "Ufaransa inaweka mfano - tumefanya hivyo kifedha kwa kutoa dola 125 milioni. Lakini mbali ya msaada wa mali, utu ndio muhimu zaidi. Na Guinea inapochukua hatua za kuuguza na kuzuwia Ebola isisambae, hivyo inasaidia uli

rais kikwete apona saratani

Image
  Rais Jakaya Kikwete wa Tanzania amesema amepona saratani baada ya kufanyiwa upasuaji mapema mwezi huu nchini Marekani. Kiongozi huyo wa Tanzania mwenye umri wa miaka 64 ametoa hotuba kwa taifa kuelezea afya yake.. "Niligundulika kuwa na hatua ya pili ya saratani ya kibofu, ambayo baadaye ikaonekana kuwa ni hatua ya kwanza," alisema Kikwete katika hotuba iliyotangazwa moja kwa moja kupitia televisheni akiwa uwanja wa ndege wa Dar Es Salaam baada ya kurejea kutoka Marekani. Aliongeza kuwa madaktari wamesema sasa hali yake shwari: "Madaktari walisema saratani haikuenea katika sehemu nyingine za mwili na baada ya upasuaji sasa wamesema nimepona saratani." Alisema aligundulika kuwa na saratani ya kibofu zaid ya mwaka mmoja uliopita na alifanyiwa upasuaji katika hospitali ya Johns Hopkins Hospital tarehe nane Novemba. Kikwete ambaye anamaliza muhula wake wa pili mwakani amesema wananchi wajenge tabia ya kupima afya zao ili wagund