chuo kikuu Kenya chavamiwa



 
Stori ambayo imechukua Headlines tangu asubuhi ya leo April 02 ni taarifa kutoka kwa wenzetu Kenya  kutokana na lile shambulio la kigaidi limehusishwa na kikundi cha Kigaidi cha Al-Shabaab na hii ni baada ya kuvamia Garissa College University, huu ni muendelezo wa kile kilichoripotiwa mwanzo.

Mpaka sasa ripoti inasema Wanafunzi 70, wameuawa na wengine zaidi ya 79, wamejeruhiwa kutokana na tukio la uvamizi wa  Garissa College University, wanafunzi walionusurika wamesema magaidi hao walianza kuwapiga risasi walinzi wawili waliokuwa getini na kuelekea katika mabweni ya wanafunzi ambapo walianza kuwagawa kwa dini zao na kuanza kuwaua kwa risasi.

Kufuatia tukio hilo Rais Uhuru Kenyatta, amemtaka Inspector Generali wa Polisi, Joseph Boinet kuhakikisha wanamgambo wote wanaripoti kwenye chuo cha mafunzo ili kuongeza idadi ya maafisa wa Polisi nchini humo.

Amesema taifa hilo linakubwa na uhaba wa maafisa wa Polisi kutokaza na kufutwa kwa zoezi la kuwasajili maafisa wa Polisi, Serikali ya Kenya imetangaza kumzawadia shilingi milioni ishirini za Kenya mtu yoyote atakaefanikisha kukamatwa kwa mshukiwa mkuu wa shambulio hilo anaefahamika kama Mohhamed Mahamoud, Polisi bado wanaendelea na zoezi la uokoaji.


Comments

Popular posts from this blog

hii ni list ya baadhi ya majina ya wasanii wa Nigeria waliohit mwaka huu kuanzia A-Z

mbinu za kuwa producer au mtayarishaji wa music