Boko Haram waondoka Gombe

Wapiganaji Waislamu wa Boko Haram wametoka katika mji wa Gombe kaskazini-mashariki mwa Nigeria baada ya mapambano makali na jeshi.
Wakuu wanasema wapiganaji wamerejeshwa nyuma, lakini ripoti nyengine zinasema kuwa wapiganaji hao waliondoka kwa hiari yao.
Boko Haram waliingia Jumamosi asubuhi katika vitongoje vya Gombe baada ya kushambulia mji jirani wa Dadin Kowa.
Wapiganaji hao wamewahi kufanya mashambulio ya kujitolea mhanga katika mji wa Gombe, lakini hawakupata kujaribu kuuteka mji wenyewe.
Nigeria ikitarajiwa kufanya uchaguzi tarehe 14 Februari, lakini umeakhirishwa kwa majuma sita kwa sababu ya wasiwasi kuhusu usalama.

Comments

Popular posts from this blog

hii ni list ya baadhi ya majina ya wasanii wa Nigeria waliohit mwaka huu kuanzia A-Z

mbinu za kuwa producer au mtayarishaji wa music